Kutoka Uwanja wa Mkapa
TAYARI mashabiki na wapenzi wa soka wameshaanza kuingia katika Dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushuhudia mtanange wa ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/2022 utakaopigwa uwanjani hapo baadaye leo jioni, Jumamosi, Septemba 25, 2021.
Mtanange huo wa kukata na shoka utawahusisha watani wa jadi, Simba Sc vs Yanga Sc wakiwania Ngao ya Jamii kuashiria kuanza rasmi kwa ligi hiyo.