The House of Favourite Newspapers

Kuzimu Na Duniani-21

1

ILIPOISHIA WIKI ILIYOPITA:
Nilisukuma mlango, nikazama ndani lakini nilifikia kuanguka chini na kupoteza fahamu.
SASA ENDELEA…

Niliposhtuka, nilikuwa katikati ya watu chini. Watu wenyewe ni waumini wa kanisani kwa mke wangu. Mke wangu pia alikuwepo na mchungaji wake, wote waliniangalia.

Ilionekana walikuwa wakisali, kujitokeza kwangu ndiko kuliwafanya wanyamaze. Nilipoangalia vizuri nikagundua nipo sebuleni kwangu.

“Pole sana bwana, habari za kuzimu?” aliniambia mchungaji huku akiwa ameshika Biblia.
Sikumjibu, nikainuka na kukaa kwenye kochi. Mchungaji akanisimulia kuwa, baada ya kutoweka nyumbani, mke wangu alimpa taarifa, ikabidi wafunge na kuomba kwa siku tatu na siku hiyo ndiyo ilikuwa ya tatu, wakaamua kuja kumalizia nyumbani kwa maombi mazito.

Mchungaji alisema aliona katika maono nikiwa nasulubiwa katika mikutano ya kuzimu, hivyo alizidisha maombi ili kunifungua katika kifungo hicho.

Niliwashukuru sana wote, hasa mke wangu. Mchungaji akaniambia nipige magoti ili aniongoze sala ya toba. Mpaka leo hii mimi ni muumini mzuri wa kiimani katika kanisa la kiroho analosali mke wangu, lipo mjini Iringa.

MWISHO.

1 Comment
  1. tmomas machera says

    pole sana bro

Leave A Reply