The House of Favourite Newspapers

Kwasi: Hakuna Kama Tshishimbi Yanga SC

Asante Kwasi.

BEKI mpya wa Simba, Asante Kwasi, raia wa Ghana, ameibuka na kusema kuwa, katika wachezaji wa Yanga, Papy Tshishimbi ni mfano wa kuigwa kutokana na jinsi anavyomfahamu. Kwasi ambaye aliwahi kucheza na Tshishimbi kwenye kikosi cha Mbabane Swallows ya Swaziland kabla ya msimu uliopita kuibukia Mbao FC, hivi sasa amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Lipuli FC.

 

Akizungumza na Championi Jumatatu, Kwasi alisema anachofahamu kutoka kwa Tshishimbi ni mchezaji mtulivu ndani na nje ya uwanja, lakini pia anatimiza majukumu yake ya ndani ya uwanja ipasavyo, hivyo ni mchezaji wa kipekee kikosini hapo.

Papy Tshishimbi.

“Namjua sana Tshishimbi kuliko mchezaji mwingine pale Yanga kwa sababu nimewahi kucheza naye kwenye kikosi cha Mbabane, ni mchezaji mzuri kwani anajua anatakiwa kufanya nini na wakati gani ndani ya uwanja.

 

Kutokana na hilo, naamini ataisaidia sana timu yake, lakini pia ukimkuta nje ya uwanja, ni mtulivu sana hana ile tabia ya ubabeubabe, hivyo ndivyo ninavyomfahamu huyo jamaa,” alisema Kwasi.

Omary Mdose na Martha Mboma

Comments are closed.