The House of Favourite Newspapers

Lampard Atoa Kauli Nzito Chelsea

0

ALIYEKUWA Kocha wa Chelsea, Frank Lampard, amefunguka kwa mara ya kwanza tangu alipotimuliwa na klabu hiyo jana kufuatia mwendelezo mbaya wa matokeo ya ligi mbalimbali ambazo timu hiyo imekuwa ikishiriki.

 

“Imekuwa fursa kubwa na heshima kusimamia Chelsea, klabu ambayo imekuwa sehemu kubwa ya maisha yangu kwa muda mrefu. Kwanza, ningependa kuwashukuru mashabiki kwa jinsi walivyonisapoti na kunipokea katika miezi 18 iliyopita.

 

“Ninajivunia mafanikio ambayo tulipata, na ninajivunia wachezaji wa akademi ambao wameingia katika kikosi cha kwanza na wamefanya vizuri sana.

 

“Nataka kumshukuru Bwana Abramovich, bodi, wachezaji na timu kila mmoja katika klabu kwa bidii na kujitolea, hasa katika nyakati hizi ambazo hazijawahi kutokea na zenye changamoto. Naitakia kila la heri timu ( Chelsea) na mafanikio kuko mbele,” amesema Lampard.

 

 

Leave A Reply