The House of Favourite Newspapers

LAZIMA SAJENTI AMZALIE DULLAH MAKABILA

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Husna Idd ‘Sajenti’ ameapa kuwa lazima ampatie japo mtoto mmoja staa wa Singeli, Abdallah Makabila ‘Dullah Makabila’.

Sajenti aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, pamoja na kwamba miezi michache iliyopita alipata balaa baada ya ujauzito wake kutoka, lakini bado anaamini Mungu atamsaidia, atapata mwingine.

“Ninamuomba sana Mungu anifanikishe tena kwani nimepanga lazima nimzalie Dullah (Makabila),” alisema Sajenti.

Sajenti aliongeza kuwa, Dullah anapenda watoto na hilo ndilo lililomhamasisha zaidi kutamani kumpatia mtoto.

STORI: IMELDA MTEMA, DAR

Comments are closed.