The House of Favourite Newspapers

Lebron Apigwa Zengwe Tuzo Ya MVP

0

ZENGWE limenza kupigwa juu ya nani anastahili kuwa mchezaji bora wa msimu wa Ligi Kuu ya Kikapu Marekani (NBA), huku staa Lebron James akionekana kupigwa kikumbo.

 

Uchunguzi wa Kampuni ya ESPN umebaini kuwa wajumbe 10 wa kamati ya tuzo hiyo wanawatazama zaidi Kevin Durrant ambaye ni shujaa wa timu ya Taifa ya Marekani na klabu ya Brooklyn Nets.

 

Wengine ni Giannis Antetokounmpo ambaye ameisaidia klabu ya Milwaukee Bucks kuchukua ubingwa wake wa kwanza wa NBA baada ya miaka 50 kupita.Baada ya harakati hizo kumfikia Lebron mwenyewe, inatajwa ameanza kujipigia debe huko twitter na kuna nyakati amekuwa akiandika maneno yenye mafumbo

Leave A Reply