The House of Favourite Newspapers

Lewandowski, Klopp, Manuel Neuer Wanyakua Tuzo Bora za FIFA

0

ROBERT Lewandowski, mshambuliaji nyota wa Bayern Munich ameshinda tuzo ya mwanasoka bora wa Fifa huko Zurich na kuwashinda washindi wa miaka iliyotangulia, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

 

Mshambuliaji huyo kutoka Poland alifunga mabao 55 katika michezo 47 tu msimu uliopita na kuisaidia miamba ya Ujerumani Bayern Munich kunyakua mataji matatu katika msimu moja, yaani kombe la ligi ya Ujerumani, kombe la taifa na ligi ya mabingwa ulaya.

 

Lewandowski mwenye umri wa miaka 32, alimaliza msimu akiwa mfungaji bora wa ligi, kombe la taifa na Ligi ya Mabingwa.

 

Mlinzi wa Manchester City, Lucy Bronze, alishinda tuzo ya mchezaji bora wa wanawake. Washindi waliamuliwa na uteuzi kutoka kwa manahodha wa timu za mataifa na makocha wakuu, kura ya mtandaoni ya mashabiki na wawakilishi 200 wa vyombo vya habari.

 

Hii ni mara ya kwanza kwa Lewandowski kushinda tuzo hiyo, mbali na mshambuliaji wa Barcelona Messi au Ronaldo wa Juventus ambao wamekuwa wakipishana kushinda.

 

Msimu huu, Lewandowski amechukuliwa kutoka alipoishia na mabao 16 katika michezo 14 aliyoichezea Bayern.

 

“Ikiwa utashinda tuzo kama hii na kuwa na taji linalohifadhiwa pia na akina Messi na Ronaldo, hiyo haiwezekani na ina maana kubwa kwangu,” Lewandowski alisema na kuongeza:

 

“Miaka iliyopita, nakumbuka nilikuwa nikitamani kitu kama hiki na sasa ninaweza kushinda tuzo kama hii. Hii inamaanisha, bila kujali unatoka wapi, yote muhimu ni bidii uliyoifanya.”

Klopp ashinda tuzo ya kocha bora tena

Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp alitambuliwa kwa kuiongoza Liverpool kutwaa taji lao la kwanza la Ligi Kuu kwa kuteuliwa kuwa kocha bora wa wanaume kwa mwaka wa pili mfululizo.

 

Mjerumani huyo alishinda tuzo hiyo mnamo mwaka 2019 baada ya kutwaa Ligi ya Mabingwa na Liverpool na kumshinda kocha wa Bayern Munich Hansi Flick na Mkufunzi wa Leeds United , Marcelo Bielsa kwa tuzo ya juu mwaka huu.

 

“Nimeshtuka,” Klopp alisema.

“Nina watu wengi sana wa kuwashukuru na zaidi ya wasaidizi wangu wote. Ikiwa ningejua kuwa nitashinda ,wasaidizi wangu wangekuwa nami hapa. Kile tulichofanya mwaka jana ni juu ya vijana hawa.”

Neuer atajwa kipa bora

Kulikuwa na mafanikio zaidi kwa Bayern Munich kwani Manuel Neuer alishinda tuzo ya kipa bora wa wanaume, akiwashinda Jan Oblak wa Atletico Madrid na Alisson wa Liverpool.

 

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani aliingizwa mabao 31 tu katika michezo 33 aliyoichezea Bayern kwenye Bundesliga na akaokoa idadi kubwa ya michomo katika hatua za mtoano za Ligi ya Mabingwa Ulaya kusaidia timu yake kufika na kutwaa fainali.

Leave A Reply