Licha ya Kuandamwa… R KELLY SHOO KAMA KAWA
LICHA ya sakata lake la unyanyasaji wa mabinti kingono kuendelea kuwa juu kila kona, mkongwe wa R&B, R Kelly, ameibuka na kutangaza kufanya ziara barani Ulaya.
R Kelly ameamua kuchukua jukumu hilo kupitia mi tandao y a kijamii na kueleza mpango wake wa ziara ya muziki katika nchi ya Australia, New Zealand na Sri Lanka. Pia amepanga kufanya shoo nchini Ujerumani mwe z i Aprili, mwaka huu.
Mipango hiyo ime kuja baada ya R Kelly kukataa mashtaka yanayomkabili dhidi yake na kwamba hakuwa na hatia ya uhalifu wowote wa kingono, licha ya ‘documentary’ ya Surviving R Kelly iliyodondoka mtaani ikionesha namna jamaa alivyokuwa anafanya unyanyasaji wa kijinsia, kimwili na kiakili kwa wasichana wenye umri wa chini ya miaka 18.
NEW YORK, Marekani.
Comments are closed.