The House of Favourite Newspapers

Video: Mkutano Mkuu Wa TFF Wafanyika Tanga

0

LEO Agosti 7, 2021 ni siku ya uchaguzi wa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) ambao unatarajiwa kufanyika jijini Tanga.

 

Ni nafasi ya Urais ambapo Wallace Karia anatarajiwa kuthibitishwa na wajumbe kwa sababu jina lake lilipita peke yake kwenye mchujo.

Wale wengine ambao walikuwa wanagombea nafasi hiyo walishindwa kupenya kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kushindwa kukidhi vigezo.

Wajumbe ni 17 ambao wanawania nafasi kwenye uongozi TFF. Kwa mujibu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) Wakili Kiomoni Kibamba amesema kuwa kila kitu kipo sawa kwa ajili ya uchaguzi.

 

“Ikifika saa 9:00 mchana Watanzania watakuwa wameshajua ni viongozi gani watakuwa wamepata nafsi ya kuongoza mpira wetu kwa miaka minne, maandalizi yote yamekwisha kamilika,” amesema.

Leave A Reply