The House of Favourite Newspapers

FT: SportPesa Cup; Everton 2-1 Gor Mahia

0
Wachezaji wa timu ya Everton wakipasha kabla ya mechi yao dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.

FT: Everton 2-1 Gor Mahia

Dakika ya 90: Mwamuzi wa akiba anaonyesha dakika 6 za nyongeza

Dakika ya 87: Gor Mahia wanarudi nyuma kuzuia.

Dakika ya 82: Everton wanapata bao la pili kupitia kwa Kieran Dowell ambaye anawatoka walinzi wa Gor Mahia na kupiga shutli ambalo limejaa wavuni moja kwa moja.

GOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO

Dakika ya 81: Shambulizi lingine kali langoni mwa Gor Mahia lakini mpira unagonga mwamba na kutoka nje.

Dakika ya 76: Everton wanapata kona, inapigwa ndegu na kupigwa kichwa lakini inatoka nje inakuwa goal kick.

Dakika ya 70: Kasi ya mchezo imeongezeka upande wa Everton, wanafanya mshambulizi mara kadhaa.

Dakika ya 65: Everton wanafanya shambulizi kali lakini wanakosa umakini mpira unatoka nje.

Dakika ya 65: Everton wanafanya shambulizi kali lakini wanakosa umakini mpira unatoka nje.

Dakika ya 55: Kumbuka matokeo bado ni 1-1, Kocha wa Everton, Dylan Kerr anatoa maelekezo mara kadhaa kwa wachezaji wake.

Dakika ya 53: Kasi inaendelea na sasa Everton wanaonekana kujipanga zaidi kwa kutengeneza nafasi kadhaa.

Dakika ya 49: Kasi ya mchezo inaendelea lakini siyo kubwa kama ilivyokuwa kipinsi cha kwanza.

Kipindi cha pili kimeanza.

MAPUMZIKO

HT: Mapumziko bado Everton 1-1 Gor Mahia

45; Bado dakika moja timu ziende mapumziko, huku wakiendelea kushambuliana kwa kasi

Dakika ya 39: Timu zote zinaendelea kushambuliana kwa zamu, mabao bado moja moja

Dakika ya 38: Goooooooooooooooo Gor Mahia wanasawazisha bao

Dakika ya 34 Goooooooooooooooooooooooo Rooney anafunga bao la kwanza

Dakika ya 30, Everton wanaongoza kwa kumiliki mpira huku Rooney akiendelea kudhibitiwa vikali.

Dakika ya 27 bado Rooney hajaonesha makali yake kama alivyodhaniwa na wengi timu ya Gor Mahia wanaonekana kuwadhibiti Everton.

Dakika ya 16 bado timu zote zinashambuliana kwa zamu,

Dakika ya 12 bado Everton 0-0 Gor Mahia.

Kikosi cha timu ya Everton kilichoanza dhidi ya Gor Mahia.
Kikosi cha Gor Mahia kilichoanza leo dhidi ya timu ya Everton.

Wachezaji wa Everton wakiingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo. #EvertonInTZ

A post shared by Global Publishers (@globalpublishers) on

 

PICHA: RICHARD BUKOS NA MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS

TAZAMA MKWAJU WA ROPONEY UKIZAMA WAVUNI

Leave A Reply