Liverpool Yaisambaratisha Atalanta Uefa Champions
MECHI za hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa msimu huu 2020/21 zinaendelea kuchezwa kwenye viwanja mbalimbali.
Usiku wa jana Novemba 3 2020, zilichezwa jumla ya mechi nane na kushuhudia vipigo vizito. Ni mechi tatu pekee ndizo zimemalizika kwa ushindi wa magoli mengi ambapo ni mechi ya Shakhtar wakiwa nyumbani wamefungwa 0-6 na Mönchengladbach, RB Salzburg wakiwa nyumbani kwao wamefungwa 2-6 na Bayern Munich huku Liverpool nao wakiwa ugenini wameichapa Atalanta 5-0.