The House of Favourite Newspapers

Logarusic apiga simu kuomba kazi Simba SC

0

Nicodemus Jonas, Dar es Salaam

KOCHA mwenye mbwembwe nyingi, Zdravko Logarusic, kwa sasa yupo nyumbani kwao Croatia baada ya kuzinguana na Wakenya wa FC Leopards, sasa anasema anasaka timu popote pale hata iwe timu yake ya Simba iliyomtimua.

Ikumbukwe kuwa Loga alitimuliwa na Simba mwishoni mwa msimu wa 2013/14, katika maandalizi ya  msimu uliopita na timu kupewa Mzambia, Patrick Phiri ambaye pia alitimuliwa ndani ya mechi nane, kisha kuwa mikononi mwa Mserbia, Goran Kopunovic kabla ya kukabidhi kijiti kwa Muingereza, Dylan Kerr.

Akizungumza na Championi Jumatano akiwa kwao Croatia, Logarusic alisema licha ya Simba kumtimua, anaamini ni sehemu ya maisha ya ukocha na kwamba yupo tayari kurejea kikosini hapo.

Ameongeza kuwa mbali na hilo, pia bado anapenda maisha ya Tanzania kutokana na kujaliwa vipaji vya soka.

“Kwa sasa niko Croatia ninapumzika, sina timu, lakini nikipata ofa popote pale nipo tayari kufanya kazi. Hata kama ni kurudi Simba nipo tayari, maana sina uhasama nao, sema ni sehemu ya maisha ya ukocha kuachishwa kazi. Naipenda Tanzania, nafurahia sana maisha ya hapo kutokana na kujaliwa kuwa na vipaji vya soka. Kweli naipenda Tanzania,” alisema Logarusic.

Leave A Reply