The House of Favourite Newspapers

Lowassa Amtembelea Lissu Hospitalini Nairobi

0
Lowassa akiwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, dereva wa Lissu (kulia), kushoto ni mke wa Tundu Lissu.

MMOJA wa viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia alikuwa mgombea wa urais katika uchaguzi uliopita, Edward Lowassa, leo amemtembelea Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, anayetibiwa jijini Nairobi baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mjini Dodoma wiki iliyopita.

Ujumbe wa Lowassa ambao ameuweka kwenye mtandao wa Twitter unasema kwa Kiingereza kwamba: Earlier today i paid a visit at Nairobi Hospital to see our MP, President of TLS and dear friend (Mapema leo nilikwenda Hospitali ya Nairobi kumwona Mbunge na Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika (TLS) ambaye ni rafiki yangu mkubwa.)

Lissu alishambuliwa na kujeruhiwa vibaya kwa risasi na watu ambao hawajulikani alipokuwa anarejea nyumbani kwake mchana baada ya kikao bungeni ambapo alikimbizwa Hospitali ya Dodoma na hatimaye Nairobi kwa matibabu zaidi.

 

Breaking News: Rais Magufuli Agoma Kusaini Waliohukumiwa Kunyongwa

Leave A Reply