The House of Favourite Newspapers

Lulu Amber Agoma Kufuta Tatuu ya Young D

0
Video Queen anayesumbua Bongo, Lulu Augen ‘Amber Lulu’ .

Na Ally Katalambula | IJUMAA | Story Mix

VIDEO Queen anayesumbua Bongo, Lulu Augen ‘Amber Lulu’ ameweka wazi kuwa, pamoja na kwamba kwa sasa msanii wa Bongo Fleva, David Genzi ‘Young D’ hana mpango naye, hatafuta tatuu yake kwa kuwa inabaki kama kumbukumbu maishani kwake.

Akizungumza na Story Mix, Amber anayefanya pia Muziki wa Bongo Fleva akiwa na Ngoma ya Watakoma alisema, tatuu hiyo yenye jina la Young D iliopo upande wake wa kushoto ni kumbukumbu tosha ya maisha yake. “Sina mpango wa kuifuta tatuu ya mwanaume niliyempenda, hata mwanaume ajaye atalazimika kulifahamu hilo, siwezi kuifuta eti kisa hanitaki, hii itabaki mwilini mwangu daima,” alisema Amber Lulu.

Leave A Reply