Na Andrew Carlos | IJUMAA| ShowBiz
MWANAMUZIKI anayefanya poa kwa sasa katika Bongo Fleva na Ngoma ya Milele, Lulu Abas ‘Lulu Diva’ amenasa katika penzi la msanii kutoka Zimbabwe, Mukudzeyi Mukombe ‘Jah Prayzah’ na kwamba wawili hao wamekuwa wakijiachia bila wasiwasi.
Chanzo kiliitonya Showbiz kuwa, Lulu Diva aliyewahi kuwa video queen kwenye video mbalimbali na kuacha, amekuwa akisafiri mara kwa mara kwenda Zimbabwe na hata msanii huyo huwa anakuja kwa siri nchini.
“Mapenzi yao hayana kificho kwani Lulu kwa sasa ameamua kuachana na mapenzi ya Kibongo ambayo anaona kama ni ya kitapeli,” kilisema chanzo. Showbiz baada ya kunasa picha za wawili hao, ilimtafuta Lulu na kumhoji juu ya ishu hii ambapo alifunguka:
“Hizo habari kama unavyosikia ndiyo hivyo. Kwa sasa nimeamua kutulia na Jah (Prayzah) wangu na mbali na uhusiano, amekuwa akinionesha njia nzuri za kimuziki,” alisema Lulu.
Jah Prayzah anatamba na Wimbo wa Watora Mari aliomshirikisha staa wa muziki, Diamond Platnumz.
Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam
Comments are closed.