The House of Favourite Newspapers

LULU DIVA: NISINGEJIONGEZA, NINGEJIUZA!

Lulu Abbas ‘Lulu Diva’

MWANAMUZIKI anayefanya vizuri kwa sasa ambaye pia ni muigizaji, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amefunguka kuwa kama asingetumua akili ya kuamua kujituma kwenye muziki, angeweza kujiingiza kwenye biashara ya kujiuza.

 

Akizungumza na Amani, Lulu Diva alisema endapo asingejiongeza, halafu akakumbana na hali hii ngumu ya sasa kwa wasiokuwa na kazi, lazima angeshawishika kufanya biashara hiyo haramu.

 

“Niliwahi kufanya kazi kwenye mgahawa pale Mlimani City, nikaacha ili nipambane kwa kuwa nilikuwa nalipwa kidogo hivyo nisingetumia akili hata ya kufikiria kuimba ningeweza hata kujiuza katika hali ya sasa,” alisema Lulu ambaye mbali na muziki pia anaigiza na amefanya vyema kwenye filamu ya Nikabu ya Mussa Kitale ‘Mkude Simba’.

Comments are closed.