The House of Favourite Newspapers

Lwandamina: Tunaipiga KMC, Tunaishusha Yanga

0

MANJIRO LYIMO, Dar: KOCHA Mkuu wa Azam, George Lwandamina, amesema kuwa kuelekea kwenye mchezo wa leo dhidi ya KMC FC, ana imani kubwa na wachezaji wake katika kupata alama tatu zitakazoipandisha timu kwenda nafasi ya pili na kuishusha Yanga SC.

 

Ikiwa katika nafasi ya tatu kwa pointi 54, Azam FC itafanikiwa kuikuta Yanga SC iliyopo nafasi ya pili kwa pointi 57 watakapocheza leo lama watapata alama tatu kwenye mchezo dhidi ya KMC.

 

Akizungumza na Championi Jumamosi, Lwandamina alisema kuwa kwenda kwenye mechi inayofuata wanahitaji kuwa na ufanisi sana kwa sababu hautakuwa mchezo rahisi ila watajitahidi wapate alama tatu na kufunga mabao mengi ili waweze kuipata nafasi ya pili kwenye msimamo.

 

“Katika mpira wa miguu chochote kinawezekana. Kwa hivyo, kwenda kwenye mechi inayofuata ya KMC FC tunafahamu kwamba tunahitaji kuwa na ufanisi sana kwa sababu hautakuwa mchezo rahisi.

 

“Wachezaji wangu wapo vizuri. Wanajua wazi kuwa kilicho muhimu kwa kila mchezaji ambao wana nafasi ya kuifanya timu ipande ni ufanisi. Dube (Prince), Lyanga (Ayoub), Nado (Idd) na wengine kwa mazoezi tunayoendelea kuyafanya, nina imani nao wote kuwa wataipandisha timu katika nafasi ya pili,” alisema.

Leave A Reply