Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (TAMISEMI), George Simbachawene, (katikati), akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili kwa wakuu wa wilaya wastaafu iliyoandaliwa na PSPF na kufanyika Agosti 15, 2016. Waziri Simbachawene alimwakilisha Rais John Magufuli. Wenine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt.Ashantu Kijaji,Mwenyekiti wa Wakuu hao wa Wilaya wastaafu, Ramadhan Maneno, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSPF, George Yambesi, na Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), George Simbachawene, (kulia), akifurahia jambo baada ya kukabidhiwa kadi ya uanachama wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kupitia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko huo, George Yambesi. Waziri Simbachawene, alijiunga na Mfuko huo mara baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili ya ujasiriamali kwa wakuu wa
wilaya wastaafu na maafisa wastaafu wa serikali kwa niaba ya Rais John Magufuli jijini Dar es Salaam Agosti 15, 2016.