The House of Favourite Newspapers

Maafande Wawabananisha Yanga

0

 

LICHA ya nyota wao Fiston Abdulazack, kupachika bao la kuongoza kipindi cha kwanza dakika ya 41 halikuwafanya Yanga kusepa na pointi tatu, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

 

Fiston alipachika bao hilo la kwanza kwa kisigino mbele ya Kelvin Yondani ambaye aliamini kwamba nyota huyo ameotea ila mwamuzi Mwinyimkuu Abdalah aliweka mpira kati.

 

 

Mpaka dakika 45 zinakamilika ubao ulikuwa unasoma Polisi Tanzania 0-1 Yanga na kuwafanya vinara hao wa ligi kuingia kipindi cha pili kwa kujiamini.

 

 

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo timu zote mbili zilikuwa zinashambuliana kwa zamu na iliwabidi Polisi Tanzania wasubiri mpaka dakika ya 89 kupachika bao la kuongoza.

 

 

Ilikuwa ni kupitia kichwa cha Pius Buswita ambaye aliweka mzani sawa kwa mpira wa faulo ya Cosmas na kuizamisha mazima nyavuni.

 

 

Licha ya kuwa walikuwa pungufu Polisi Tanzania kwa kuwa beki wao kisiki Kelvin Yondani alionyeshwa kadi mbili za njano na kufanya aonyeshwe kadi nyekundu.

 

 

Sare hiyo inafanya Polisi Tanzania kufikisha pointi 29 ma ipo nafasi ya nane huku Yanga ikiwa na pointi 50 imecheza jumla ya mechi 23.

 

 

Pia kikosi cha Yanga leo kilikuwa na mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kurejea kwa nyota wao Ditram Nchimbi ambaye alikuwa anapambana na timu yake ya zamani ya Polisi Tanzania.

Leave A Reply