The House of Favourite Newspapers

Mabao yamrejesha Kiiza ‘The Cranes’

0

HAMISI-KIIZA.jpgMshambuliaji tegemeo hivi sasa Simba, Hamis Kiiza.

Wilbert Molandi,
Dar es Salaam
KOCHA Mkuu wa Timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’ Mserbia, Milutin Sredojevic ‘Micho’ amemuita mshambuliaji tegemeo hivi sasa Simba, Hamis Kiiza kwenye kikosi chake.

Timu hiyo, kwa sasa ipo kwenye maandalizi ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Afrika (Afcon) na Kombe la Dunia 2018.
Kiiza ameitwa kwenye kikosi hicho ikiwa ni baada ya kuifungia timu yake ya Simba mabao nane hadi mpaka sasa katika Ligi Kuu Bara.
Akizungumza na Championi Jumatano, Kiiza alisema tayari wamepokea barua ya mwaliko wa kujiunga na kikosi hicho pamoja na beki kisiki wa Simba, Juuko Murshid.
Kiiza alisema, wanatarajia kuelekea kwao Uganda wakati wowote kuanzia sasa mara watakapotumiwa tiketi za ndege.
“Kikubwa ninashukuru sana kuitwa timu ya taifa, kwa sababu hiyo inajenga heshima na thamani yangu kwenye klabu yangu ya Simba.
“Nafikiri nimeitwa timu ya taifa ni kutokana na uwezo wangu mkubwa niliouonyesha ndani ya uwanja katika ufungaji mabao na hiyo ndiyo kazi ya mshambuliaji anayotakiwa kuifanya.
“Ninakwenda kujiunga na timu ya taifa nikiwa nimetokea kwenye majeraha, hivyo nikiwa huko nitaitumikia timu yangu ya taifa kwa tahadhari kubwa,” alisema Kiiza.

Leave A Reply