The House of Favourite Newspapers

Mabosi Azam Wamgeukia Sure Boy

0

BAADA ya Jumanne wiki hii kumsainisha mkataba wa miaka miwili mshambuliaji wao, Prince Dube, uongozi wa Azam sasa upo kwenye mazungumzo na kiungo mshambuliaji wao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ kwa ajili ya kumpa mkataba mpya.

 

Mkataba wa Sure Boy na Azam unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu, baada ya kiungo huyo kuhudumu ndani ya kikosi hicho kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10.

 

Kiungo huyo amekuwa akihusishwa na klabu mbalimbali, ambapo mwanzoni mwa msimu huu uongozi wa Yanga ulifanya jitihada za kumsajili lakini dili hilo likayeyuka baada ya pande hizo mbili kushindwana kwenye ada ya uhamisho.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Azam, Zakaria Thabith ‘Zaka Zakazi’ alisema:

 

“Baada ya kukamilisha makubaliano na mshambuliaji wetu Dube, uongozi sasa uko kwenye mazungumzo na wachezaji wetu wote ambao mikataba yao inaelekea ukingoni, ili kufanya maboresho kwenye mikataba yao na kuwapa mikataba mipya.

 

Katika mchakato huu yupo pia kiungo mshambuliaji wetu Sure Boy, ambaye ni mchezaji mwandamizi na uongozi una matumaini makubwa ya kumbakisha pamoja na nyota wetu wote.

Stori na Joel Thomas, Dar es Salaam

Leave A Reply