The House of Favourite Newspapers

Macho Yamtesa Wastara Atamani Kuhama Insta!

0
Wastara Juma

STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ameibuka na kueleza jinsi macho yake yanavyomtesa kwani watu wamekuwa wakimsema vibaya kuwa anajilegeza makusudi akitaka kutupia picha mtandaoni.

 

Akipiga stori na Risasi Jumamosi,Wastara alisema kuwa macho yake ndivyo yalivyo kwani amezaliwa hivyo ni macho yaliyolegea kama mtu mwenye usingizi wakati wote na kutokana na vichambo anavyovipata amejikuta akitamani kuhama Insta lakini hawezi kwa sababu ana manufaa na page yake.

 

“Jamani haya macho yananitesa kwani kutwa kucha natukanwa mitandaoni kuwa nalegeza macho hawajui kuwa nimeumbwa hivi kwani hata nikijitahidi kuyafanya yawe magumu nashindwa, hivyo watu wakisema najifanyisha huwa najisikia vibaya kusema ukweli,” alisema Wastara.

Leave A Reply