The House of Favourite Newspapers

MADEE afungukia kuchambwa na Wolper

0
MADEE afungukia kuchambwa
Hamadi All ‘Madee’

BAADA ya kumwagiwa mkwara mzito, Rais wa Manzese ambaye pia ni mkali katika Muziki wa Bongo Fleva, Hamadi All ‘Madee’ amefungukia ishu ya kuchambwa na msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper kuwa alikuwa sahihi kumchamba kwa kuwa alitumia picha ya katuni inayofanania na yeye bila kumuomba.

 

 

MADEE afungukia kuchambwa

Madee afungukia kuchambwa

Akizungumza na Showbiz, Madee alisema, wakati wa kutengeneza video yake mpya ya Sikila aliyomshirikisha staa kutoka Nigeria, Tekno yenye muonekano wa kikatuni, mchoraji alipendekeza kutumia msichana mweupe na mwenye sifa tofautitofauti hivyo wazo likamjia la kumtumia Wolper. “Nilikosea kumtumia Wolper kwa sababu kwanza sikumuomba.

 

Wolper.

Wolper ni mshkaji nitawasiliana naye ili tuweze kulimaliza,” alisema Madee. Juzikati kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wolper alimchamba Madee kwa kumtumia muonekano wa kikatuni katika wimbo wake.

NA: IRENE MNYITAFU| IJUMAA

 

VIDEO: ROMA Alivyowasili Tanzania Akitokea Zimbabwe

Leave A Reply