Magufuli aahidi neema kwa Wanabukoba
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, Dk. Jonh Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Bukoba, mkoani Kagera jana.
Chege na Temba wakiwaburudisha wakazi wa Bukoba wakati wa mkutano huo.
Wakazi wa Bukoba wakimsikiliza kwa makini Dk. Magufuli.
Diamond na wanenguaji wake wakifanya yao jukwaani.
Dk. Magufuli akitoa pole kwenye msiba wa aliyekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya CCM, kata ya Muleba Bw. Osward Peter Rwakabwa.
Aliyekuwa mgombea udiwani kwa tiketi ya CCM, kata ya Muleba Bw. Osward Peter Rwakabwa, enzi za uhai wake.
farid kubanda, Fid Q, akifanya yake.
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli jana aliingia mkoani Kagera kuendelea na mikutano ya kampeni katika maeneo mbalimbali ya mkoani humo, moja ya mikutano hiyo ni ule uliofanyika Bukoba mjini.
Katika mkutano huo, Dk. Magufuli aliwaahidi wakazi wa jimbo la Bukoba Mjini kuwa, katika Ilani ya Uchaguzi ya 2015-2020 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamepanga kununua meli mbili mpya kwa ajili ya kutumika katika usafirishaji katika Ziwa Victoria.
Pia aliowaahidi kuwa, endapo watamchagua Magufuli kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atapunguza ushuru katika zao la kahawa ambayo ili kuwafanya wakulima wa zao hilo kunufaika zaidi na kupitia zao hilo watakuza uchumi wao na uchumi wa Taifa.
Kutokana na kuongezeka kwa kodi, imewalazimu kuuzwa mazao hayo kwa bei ya juu ili muuzaji kufidia kodi anazochajiwa jambo ambalo linawafanya wanunuzi wakimbilie nchini Uganda ambapo hununua kahawa kama hiyo kwa bei ya chini kutokana na kutokuwa na mrundikano wa kodi ambapo zimedaiwa kufikia kodi 26 ili uweze kuisafirisha kahawa hiyo kwenda nje ya nchi.
Miongoni mwa maeneo aliyofanya mikutano leo magufuli ni pamoja na Kijiji cha Kasharunga, Rulanda wilayani Muleba, kisha alikwenda nyumbani kwa aliyekuwa mgombea udiwani wa kata ya Muleba Kijiji cha Kagabilo , aliyefariki juzi kwa ajali ya bodaboda na kutoa pole kwa wafiwa.
Baada ya hapo alikwenda uwanja wa Zimbihile ilipokata ya marehemu na kuomba kura kwa umati uliofurika kumsubili, kisha akaelekea Kamachumu, Nshamba, Kijiji cha Maruku kilichopo Jimbo la Bukoba vijijini na kumalizia kwa kufanya mkutano uliokuwa fungakazi kutokana na umati uliofurika.
NA RICHARD BUKOS/GPL ALIYEKO BUKOBA