Magufuli afunga kampeni zake kwa mkoa wa Kagera
Wakazi wa Kyerwa wakimsikiliza Dk. Jonh Pombe Magufuli wakati wa mkutano wake wa kampeni.
Magufuli akijinadi sambamba na mgombea ubunge jimbo la Ngara (CCM) Alex Gashaza.
Magufuli akipiga push-up jukwaani, ili kuwaonesha wananchi kuwa afya yake iko vizuri kulitumikia Taifa. Wananchi wa Kyerwa wakisikiliza hotuba ya Magufuli. Dk. Magufuli akiwahutubia wananchi. Magufuli oyeeeee……….!!!!
Mgombea urais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu ya tao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Jonh Pombe Magufuli, leo amemaliza kufanya kampeni zake mkoani Kagera kwa kufanya mkutano wa katika jimbo la Ngara lililopo wilayani Ngara. Mkutano huo ulihudhuriwa na umati mkubwa wa watu ambao kwa mujibu wa wenyeji, haijawahi kutokea watu kujaa kiasi hicho.
Sambamba na mkutano huo wa fungakazi, Magufuli alifanya mikutano sehemu mbalimbali ikiwemo wilayani Misenyi katika jimbo la Nkenge kwenye viwanja vya Mashujaa.
Mkutano mwingine mkubwa ulifanyika viwanja vya Kayanga wilayani Karagwe, mkutano mwingine waliofurika umati wa mkubwa wa watu ni ule wa Wilaya mpya ya Kyerwa, mwingine Kijiji cha Kaishozi, Kijiji cha Kinyamisi kabla ya kumalizia na mkutano uliofungakazi katika jimbo la Ngara ambapo Alex Gashaza anagombea Ubunge.
Picha na Richard Bukos/GPL Kagera
JIUNGE NA GLOBAL BRAKING NEWS UPATE HABARI KEMKEM ZA UCHAGUZI MKUU