The House of Favourite Newspapers

MAJALIWA AAGIZA HAYA BAADA YA RC HAPI KURIPOTI OFISINI KWAKE

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kampuni zote zinazosambaza nguzo za umeme zinatakiwa zilipe ushuru wa halmashauri wanakotoa nguzo hizo amboa ni asilimia tano ya gharama ya kila nguzo kama ilivyoelekezwa na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa.

 

Ametoa agizo hilo jana (Jumatatu, Januari 7, 2019) baada ya kupata taarifa kuhusu kampuni ya New Forest ambayo inamkataba na TANESCO wa kusambaza nguzo za umeme, kwa muda mrefu kampuni hiyo imekuwa ikikaidi kulipa ushuru wa asilimia tano ya gharama ya kila nguzo. Ushuru huo umefikia sh. bilioni 2.9 hali iliyopelekea uongozi wa mkoa kuzuia nguzo hizo zisitoke.

 

Wiki iliyopita akiwa katika ziara ya mkoa Ruvuma, Waziri Mkuu alipokea malalamiko kuhusu mkoa wa Iringa kuzuia kusambazwa kwa nguzo za umeme ndipo alipoamua kuwaita Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi pamoja na wakuu wa wilaya, wakurugenzi pamoja na wenyeviti wa halmashauri wanaotoka katika wilaya zinazozalisha nguzo.

 

Viongozi wengine waliohudhuria kikao hicho ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemevu, Jenista Mhagama, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

 

Amesema lengo la kikao hicho lilikuwa kupata ufafanuzuzi kuhusu malalamiko yaliyotolewa dhidi ya uongozi wa mkoa wa Iringa kuhusu kuzuia usafirishaji wa nguzo za umeme zinazotomika kwenye miradi ya Kusambaza Nishati ya Umeme Vijiji (REA).

 

Baada ya kupata maelezo hayo, Waziri Mkuu amemuagiza mkuu wa mkoa wa Iringa kuiandikia bili kampuni ya New Forest ili ilipe ushuru huo kuanzia Julai 2018 walipoanza kusambaza nguzo. Asilimia 90 ya nguzo za umeme nchini zinatoka Iringa. Tanzania ina viwanda tisa vya kutengeneza nguzo na kati ya viwanda hivyo vinane vipo Iringa na kimoja kipo Tanga.

 

Kampuni ilizuiwa kutoa nguzo ndani ya mkoa wa Iringa tangu Novemba 2018 hadi Januari 2019 huku ikitakiwa kulipa ushuru wa asilimia tano ya gharama ya kila nguzo ambapo ilikaa ikitaka iendelee kulipa sh. 5,000 kwa kila nguzo kama walivyokubaliana na TANESCO jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Mambo Matatu Ya Dkt.Bashiru CCM Kukubalika Kwa Wananchi

Comments are closed.