The House of Favourite Newspapers

Majimaji Watembelea Ofisi za SOKABET Sinza – Mori

0
Mratibu Mkuu wa kampuni ya kubashiri Tanzania ya SOKABET, Franco Ruhinda, akiwapokea baadhi ya wachezaji na viongozi wa timu ya Majimaji ya Songea muda mfupi baada ya kutembelea ofisi za SOKABET zilizopo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.

BAADHI ya wachezaji na viongozi wa timu ya Majimaji FC ya Songea Ruvuma, mapema leo walipata fursa ya kutembelea ofisi za wadhamini wao wakuu, kampuni ya mchezo wa kubashiri ya SOKABET zilizopo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam.

…Akisalimiana na baadhi ya wachezaji na viongozi wa Majimaji baada ya kuwasili ofisi za SOKABET.

Viongozi na wachezaji hao waliamua kutumia muda wao wa mapumziko ya wiki moja kutembelea na kuona namna ofisi za wadhamini wao zinavyojiendesha kwa kutoa huduma ya mchezo wa kubashiri kiasi cha kuwa na uwezo wa kuwadhamini.

Mmoja wa waratibu wa SOKABET, John Joseph (wa kwanza kushoto) akiwapa maelezo wachezaji na viongiozi wa Majimaji jinsi SOKABET inavyotekeleza majukumu yake.

Akizungumza ndani ya ofisi hizo, msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Nduguru, alisema waliamua kutumia siku ya leo kuwatembelea wadhamini wao hao baada ya kutoka kushiriki katika mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting uliyochezwa Jumamosi iliyopita huku wakipoteza kwa bao 2-1.

Kiongozi wa kituo cha huduma kwa wateja wa SOKABET, Lusekelo akiwapa maelezo mafupi wachezaji na viongozi wa klabu hiyo namna wanavyowasiliana na wateja wao.

“Klabu yetu ya Majimaji leo imeanza mapumziko ya muda wa wiki moja, hivyo tumeona ni vizuri tukatumia nafasi yetu ya leo kuwatembelea wadhamini wetu SOKABET kabla hatujasambaa kabisa kwani tayari kambi tumeshaivunja na kuwataka wachezaji kila mmoja atumie muda huu kufanya mambo yake ila hawa wachache tumeona ni vyema tuje nao kutembelea hapa,” alisema Ndunguru.

Franco akiwa katika pozi na baadhi ya wachezaji hao.

 

Wachezaji na viongozi wa Majimaji wakiwa katika picha ya pamoja na Franco.
Ofisa Habari wa timu ya Majimaji, Onesmo Ndunguru, akiwatambulisha wachezaji na viongozi wenzake kwa baadhi ya wafanyakazi wa SOKABET.

HABARI/PICHA: MUSA MATEJA/GLOBALPUBLISHERS

Leave A Reply