NI majanga! Inaelezwa kuwa ndege iliyopotea na straika matata Emiliano Sala inawezekana isipatikane tena baada ya kuzama ndani ya maji kwenye bonde lenye urefu wa futi 600.
Bonde hilo lililopo katika visiwa vya Alderney, Uingereza, lilitumika kwa watu kumwaga kemikali za silaha zilizotumika kwenye Vita ya Kwanza ya Dunia, pamoja na takataka nyingine za tani 17,000.
Imeelezwa kuwa ni ngumu kwa ndege hiyo kupatikana kutokana na kuzama katikati ya kemikali na takataka hizo, na hivyo kuchanganyikana, tena ukiwa ni umbali mrefu kwenda chini.
Hili linakuja baada ya rubani ambaye alikuwa na Emiliano kwenye ndege hiyo, kudaiwa kuwa hana leseni ya biashara na alikuwa na deni la pauni 18,000 (Sh mil 55).
Emiliano alipotea na ndege akiwa yeye na rubani alipokuwa akitokea Ufaransa kwenye klabu yake ya Nantes na kwenda Cardiff City England ambako al ikuwa ‘ amesinya’ (amesaini) mkataba.
LONDON, England.
Comments are closed.