Makalla Ampigia Simu Live Waziri wa Fedha Kujua Fidia za Wananchi Kipunguni



Nae Mhe Waziri Dkt Mwigulu Lameck Nchemba amekiri kufahamu jambo hilo na hata yeye amezungumza sana Mhe Mbunge wa Segerea na kweli waliahidi kulipa ila kulingana na kuingiliana kwa mambo ya kiserikali wamechelewa kulipa ila wanatoa ahadi kwamba kuanzia Mwezi wa Nane Wananchi wa Kipunguni wanataanza kulipwa Fedha zao.
Pia Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo CPA Makalla amesema katika Mkutano huo fedha zikianza kulipwa aitwe nae ashuhudie pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ili kuwadhibitishia Wananchi kuwa Serikali ya Dkt Samia ikiahidi inatekeleza.