The House of Favourite Newspapers

Makambo: Nataka Ufungaji Bora Bongo

0

MSHAMBULIAJI wa Yanga Mkongomani, Heritier Makambo amesikitika kukosa kuwafunga wapinzani wao Simba lakini ameahidi kubeba kiatu cha ufungaji bora katika msimu huu.

 

Staa huyo wa Yanga aliyeingia katika kipindi cha pili akichukua nafasi ya Fiston Mayele, alikosa bao la wazi ndani ya 18 katika dakika ya 90 ukiwa ni mchezo wa Ngao ya Jamii ambao uliisha kwa Yanga kushinda bao 1-0 dhidi ya Simba.

 

Akizungumza na Championi Jumatano, Makambo alisema kuwa anaamini uwezo wake wa kufunga mabao, hivyo Wanayanga wasubirie furaha.

 

Makambo alisema kuwa kitu cha kwanza alichokipanga katika msimu huu ni kuipa ubingwa Yanga wa Ligi Kuu Bara na Kombe la FA baada ya kuyakosa mataji hayo kwa miaka minne na kwenye mafanikio yake binafsi anautaka ufungaji bora. Soma makala yake ukurasa wa 10.

 

WILBERT MOLANDI, Dar es Salaam

Leave A Reply