The House of Favourite Newspapers

Makamu wa Rais Anusurika Kuuawa kwa Bomu

0


MAKAMU wa Rais wa Afghanistan, Amrullah Saleh, amenusurika kifo baada ya watu wanaosadikiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Taleban, kushambulia msafara wake asubuhi ya leo, Septemba 9, 2020, jijini Kabul.

Takribani watu kumi, wakiwemo wasaidizi wa karibu wa makamu huyo wa rais huyo, wamepoteza maisha katika shambulio hilo huku makamu huyo wa rais akipata majeraha madogo usoni na mikononi.

Shambulio hilo limekuja wakati serikali ya Afghanistan ikiwa inajiandaa kuanza mazungumzo na wapiganaji wa Taleban.

Leave A Reply