The House of Favourite Newspapers

Makamu wa Rais Awasili Arusha kuwa Mgeni Rasmi Kongamano la Nne la Uhuru

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro akielekea mkoani Arusha leo tarehe 20 Septemba 2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango amewasili mkoani Arusha na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro mapema leo Septemba 20, 2024.

Dkt Mpangoa anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika Kuhitimisha Kongamano la 4 la Uhuru wa Kidini la Afrika litakayofanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha Septemba 21,  2024.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Viongozi mbalimbali wakati alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro akielekea mkoani Arusha leo tarehe 20 Septemba 2024.