Makamu wa Rais Mpango Ashiriki Misa Takatifu ya Dominika ya Pili ya Pasaka Nchini Italia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango ameshiriki Misa Takatifu ya Dominika ya Pili ya Pasaka katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Rita wa Kashia, lililopo katika Mji wa Cascia nchini Italia leo tarehe 27 Aprili 2025.
