The House of Favourite Newspapers

Makamu wa Rais Nchini Argentina Cristina Kirchner Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Sita

0
Makamu wa Rais Nchini Argentina Cristina Kirchner.

Makamu wa Rais Nchini Argentina Cristina Kirchner amehukumiwa kifungo cha miaka sita (6) jela kwa matumizi mabaya wa Mali ya umma.

Siku ya Jumanne Disemba 6, 2022 Mahakama Nchini humo ilimkuta Bi. Kirchner na hatia ya ufisadi ambao aliutenda kipindi cha uongozi wake kama Rais wa Nchi hiyo kati ya mwaka 2007-2015 na kuhukumiwa kifungo cha miaka 6 jena sambamba na kupigwa marufuku ya maisha kushikilia ofisi ya umma.

Bi. Kirchner amesema hatogombea nafasi yoyote ya kisiasa baada ya kukutwa na hatia hiyo.

YANGA IWE JUA IWE MVUA NAMUNGO HATOKI, SIMBA WAWEKA WAZI MIPANGO YAO YA USAJILI | KROSI…

Leave A Reply