The House of Favourite Newspapers

Makamu wa Rais Philip Mpango Awajibu Waliomzushia Kifo “Nawaombea Msamaha Kwa Mungu Awasamehe”- Video

Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Phillip Isdor Mpango akizungumza kwenye hafla ya upokeaji wa hundi ya michango ya Maafa ya mafuriko, Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 10 Desemba, 2023.

Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Philip Mpango amewashukuru Watanzania kwa kumuombea huku akibainisha kuwa alikuwa nje ya nchi kwa shughuli maalumu takribani mwezi mmoja.

“Asanteni sana kwa kuniombea, yamesemwa mengi si ndio? Na wengine bado wanasema mimi ni mzuka..

Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Phillip Isdor Mpango akifurahia jambo na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) na Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi Dkt. Moses Kusiluka (kushoto) mara baada ya hafla fupi ya kupokea Hundi ya michango kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali kwa ajili ya Maafa yaliyotokea Katesh, Disemba 10, 2023 Ikulu Mkoani Dodoma 📸-IKULU

“Muwe na amani nipo salama nilikwenda nje kufanya shughuli malum takribani mwezi mmoja sijapungua hata kidogo si ndio?… Wapo wengi walioumizwa na maneno ambayo hayana msingi, wale waliokuwa wanatuma picha yangu na mshumaa pembeni…. wengine walisema mzee amekata moto…muda wangu bado,”amesema Dk Mpango.

Dk Mpango ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa Ledochowska Kiwanja cha Ndege mkoani Dodoma katika Ibada ya Jumapili leo Desemba 10, 2023. Ibada hiyo imeongozwa na Padre Dionis Paskal Safari.

Makamu wa Rais  Dkt. Phillip Isdor Mpango akiondoka Ikulu mara baada ya hafla fupi ya kupokea Hundi ya michango kutoka Taasisi mbalimbali kwa ajili ya Maafa ya maporomoko ya ardhi yaliyotokea Katesh, Ikulu Mkoani Dodoma tarehe 10 Desemba, 2023.