The House of Favourite Newspapers

Makocha Waipa Ufaransa Ubingwa

MAKOCHA wa zamani wa Simba, Mcroatia Zdravko Logarusic na Selemani Matola wametabiri kwamba Ufaransa inabeba Kombe la Dunia leo Jumapili kwa kuipiga Croatia kwenye mechi ya fainali ndani ya Uwanja wa Luzhniki Moscow Urusi.

 

“Wengi wanaipenda Ufaransa na wanawapa nafasi, vijana wa nchi yangu, lakini wanatakiwa kuwa makini na kupambana kuhakikisha wanafanya maajabu ingawa Ufaransa ndiyo ina nafasi,” alisema Loga ambaye ni Mcroatia anayeinoa Sudan kwa sasa.

Kwa upande wa Matola yeye alisema kuwa; “Ufaransa mimi naipa nafasi sababu ina wachezaji ambao wana uwezo wa kubadili matokeo wakati wowote tofauti na Croatia ambao wanawategemea viungo wawili tu.

Comments are closed.