MKUU wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda ametekeleza ahadi ya kutoa zawadi kwa wachezaji ambao walishinda Tuzo za Mo Simba 2019. Wachezaji hao ni Manula ambaye amempa Tsh. 10 Milioni na Kagere, Nyoni, Bocco, Kotei, Juma, Chama na Mwanahamisi ambao amewapa Tsh. 1 Milioni kwa kila mmoja.
Makonda, leo amewakabidhi pesa hizo wachezaji wa Simba leo Juni 3, 2019, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Aidha, Msemaji wa Simba Haji Manara amepatiwa Tsh Mil. 3 na mchezaji Bora wa Simba Queens, Mwanahamisi amepatiwa Tsh Mil. 2.
Comments are closed.