Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto) akiambatana na wanafamilia inayodaiwa kutapeliwa nyumba yao baada ya kuwatembelea eneo wanaloishi kwa sasa huko Kunduchi.
Mkuu wa Mkoa wa Dares Salaam, Paul Makonda amemwaga machozi alipoitembelea familia ya Stela Bujumula baada ya kuelezwa jinsi inayoishi kwa kutangatanga, kufuatia kutapeliwa nyumba yao iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam, na kuahidi kutoa msaada wa kisheria ili warejeshewe nyumba yao.
Baada ya wanafamilia hiyo kumueleza jinsi walivyotolewa kwenye nyumba yao kwa madai ya kushindwa kulipa deni la mkopo waliochukua katika Benki ya CRDB na nyumba hiyo kupigwa mnada, Makonda ambaye ametoa msaada wa vyakula kwa familia hiyo kwa ajili ya kujikimu, amesema atahakikisha sheria inachukua mkondo wake.
Akizungumza mbele ya mkuu wa mkoa, mmiliki wa nyumba hiyo, Stela Bujumula alisema kwa takribani miaka sita sasa, familia yake inateseka baada ya nyumba hiyo kupigwa mnada, katika mazingira ya liyojaa utata.
Ameitaka familia hiyo kufika ofisini kwake, Ilala jijini Dar es Salaam, Jumatatu ya Januari 29, wakiwa na nyaraka zote muhimu kwa ajili ya kuanza kulifuatilia sakata hilo kuhakikisha haki inatendeka.
…Akitoa machozi mbele ya familia hiyo.
NA DENIS MTIMA | GLOBAL PUBLISHERS
Comments are closed.