MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewaongoza mamia ya watu waliojitokeza kumuaga aliyewahi kuwa kocha wa Taifa Stars, Joel Bendera katika Viwanja vya Hospitali ya Lugalo jijini Dar ambaye anatarajiwa kuzikwa kesho Korogwe, Tanga.
Bendera aliyefariki Jumatano wiki hii katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili aliwahi kushika nyadhifa tofauti serikali ikiwemo ili ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mbunge wa Korogwe Mashariki na Mjini na baadaye kuwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro na Manyara.
Simanzi na majonzi vimetawala wakati wa kuaga mwili wa kiongozi huyo ambaye pia alikuwa mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa na Kocha Mstaafu.
MUSA MATEJA/GPL.
VIDEO YA KUAGA MWILI WA BENDERA
Comments are closed.