Mr Blue, akiimba.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, jana ameungana na maelfu ya wakazi wa jiji hilo kwenye tamasha kubwa la burudani lijulikanalo kama ‘Komaa Concert 2018’ lililoandaliwa na kituo cha utangazaji cha EFM/TV E ambapo amesema serikali ya mkoa wake itaendelea kutoa ushirikiano kwa wasanii kwa kuwa sanaa ni ajira rasmi inayowasaidia vijana wengi.
Akizungumza na maelfu ya wananchi, Makonda amewaomba waendelee kumpa ushirikiano wa kutosha Rais John Magufuli huku akipongeza maendeleo makubwa yaliyopatikana tangu serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani.
Aidha amewapongeza EFM kwa kuandaa tamasha hilo lililotoa fursa kwa wananchi wanyonge kupata burudani huku akiwakumbusha wananchi kuhakikisha wanafanya usafi wa mazingira kwenye maeneo yao wanayoishi.
Pia amewahimiza wananchi kuhakikisha wanalinda amani na usalama na kuwakumbuka kwenye maombi viongozi wote wa taifa.
Comments are closed.