Makonda Atembelea Walioathirika Na Mafuriko (Picha +Video)
Mkuu wa mkoa wa Dar es alaam, Paul Makonda leo ametembelea sehemu zilizoathiriwa na mvua kali iliyonyesha jana karibu mji mzima na kusababisha mafuriko baadhi ya sehemu. Katika ziara hiyo alianzia na Kigogo mwisho, Legho Sinza, Sweet Corner Manzese na kumalizia Jangwani.
Katika ziara hiyo alijionea uharibifu wa miundombinu kama vile barabara, madaraja, nguzo za umeme n.k. ambapo amewataka wakazi wa jiji kutojenga sehemu hatarishi.
Makonda pia aliwataka wakazi wa maeneo hayo kuacha kutupa takataka mtoni ambazo nyingi zimekuwa zikiziba madaraja na kusababisha maji kushindwa kupita kiurahisi na kurudi maeneo ya makazi.
Mkuu huyo wa mkoa pia aliwalaumu wanaochimba mchanga kwenye mito na kusema hao ndiyo chanzo cha mmomonyoko wa udongo na uharibifu wa mazingira.
Mafuriko pia yamesababisha kujaa tope katika barabara Morogoro eneo la Jangwani na hali iliyopelekea barabara hiyo kufungwa ili kupisha zoezi la kuondoa tope kwenye barabara hiyo.
Wanahabari wetu wakiwa eneo hilo walishuhudia greda likisafisha barabara hiyo kwa kuondoa tope lililojaa kwenye barabara hiyo.
HABARI: RICHARD BUKOS