MAKONDA AYAONYA MAKAMPUNI YA UDALALI KUTOTUMIA NGUVU
Baadhi ya wamiliki wa makampuni ya udalali ya jijini Dar es Salaam wakimsikiliza mkuu wa mkoa, Paul Makonda (hayupo pichani).
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewataka wamiliki wa makampuni ya udalali jijini Dar es Salaam, kufuata taratibu za kisheria wanapokuwa katika majukumu yao ya kikazi katika kukamata au kuondoa mali za watu wanapokuwa wakidaiwa.
Amewaomba pia kuwaelimisha, badala ya kuwapiga viboko waendesha bodaboda wanapokuwa wakitaka kuingia maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam. Pia amewataka wawasilishe leo nyaraka zao za utambulisho wa kufanya kazi hizo zinazowaonyesha kuwa wao ni halali ili kuondoa makundi ya watu wanaojipenyeza na kujifanya ndiyo wamiliki wa makampuni ya udalali.
NA DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.