The House of Favourite Newspapers

Malaika: Mapenzi tena Bongo ‘NO’

0

MALAIKA

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Diana Exavery ’Malaika’ amefunguka kuwa kwa sasa hataki tena mpenzi Bongo badala yake akitokea mtu kutoka nje ya nchi, yuko radhi kuwa naye.

Akizungumza na Risasi Vibes, Malaika ambaye hivi karibuni alimwagana na mpenzi wake Mbongo, anayefahamika kwa jina moja la Dadi, alisema wanaume wengi wa Tanzania ni pasua kichwa, jambo linalomfanya ajaribu nje kuona

 upepo unavyokwenda.

“Sitaki tena mpenzi wa hapa kwa sasa, maana wengi wana tabia zinazofanana, lakini akitokea mtu wa nje poa, naweza kuwa naye,” alisema msanii huyo.

Leave A Reply