Mama Mzazi wa Waziri Dotto Biteko, Bi. Elizabeth Biteko Afariki Dunia
Mama mzazi wa Waziri wa Madini na mgombea wa nafasi ya ubunge katika jimbo la Bukombe Dotto Biteko, Bi. Elizabeth Biteko amefariki dunia katika hospitali ya kumbukumbu ya Charles Kulwa iliyopo Wilayani Bukombe ambako alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.