The House of Favourite Newspapers

Mama wa Mwanafunzi Aliyechapwa Kinyama na Mwalimu Mkuu Afunguka – Video

0


Tukio ni la kweli limetokea,tarehe 10.01.2023, ambapo Mwalimu huyo alipiga viboko wanafunzi zaidi ya mmoja, upigaji wake ndio ulioleta taharuki kwa umma ya Watanzania. Zaidi katika video ile kuna baadhi ya walimu waliokuwa pembeni walisikika wakicheka wakati mwalimu huyo akiwapiga wanafunzi.

Mwalimu aliyepiga viboko wanafunzi ni Mwalimu Isaya Benjamin Emmanuel, mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kakanja na walimu walioonekana na kusikika kufurahia tukio hilo wakati mwalimu Mkuu akiwachapa wanafunzi hao walikuwa ni walimu wanne ambao ni Mwalimu Godson Rwabisho,Beatrice Oswald Kaburanyange,James Josiah na Delphina Leonce.

Wanafunzi waliochapwa ni Salmon Kakwezi darasa la nne umri wa miaka tisa na Anord Kweyamba darasa la nne umri miaka kumi. Mwalimu aliwachapa viboko wanafunzi kwasababu hawakufanya kazi ya nyumbani waliyopewa wakati wa likizo akaona adhabu kubwa ya kuwaadhibu ni kuwachapa wanafunzi namna alivyowachapa.

Leave A Reply