The House of Favourite Newspapers

Mambo 12 wasiyopenda wanaume!

0

Assalam aleikum msomaji wangu, bila shaka unaendelea vema na maisha yako sambamba na maandalizi ya kuelekea uchaguzi mkuu ambao zimebaki siku chache ili kumchagua yule unayeona anafaa kuliongoza taifa hili.

Bila kuwachosha niende moja kwa moja kwenye mada ya wiki hii ambayo inahusu mambo 12 wasiyoyapenda wanaume kwa wapenzi au wake zao.

Kujipamba kupitiliza

Mwanamke kama mwanamke ni mapambo na ili awe mwanamke anao ulazima wa kuhakikisha anaonekana smati kwa kujipamba lakini si kama wafanyavyo wanawake wa siku hizi.

Wanaume wengi wamejikuta wanachukizwa na hali ya mwanamke kujipamba kupitiliza.

Yaani unakuta mwanamke anajipamba utadhani siku hiyo ni siku yake ya kufunga ndoa, hilo ni tatizo na husababisha hata mwanaume kuogopa kuongozana naye.

Sasa je, kama unatoka na mume au mpenzi wako, unajipamba hivyo kumfurahisha nani hasa? Mbona ukiwa nyumbani unakuwa wa kawaida tu?

Matumizi makubwa ya fedha

Mwanamke mwenye matumizi makubwa ya fedha ambaye hafikirii kesho itakuwaje ni adui mkubwa wa mwanaume.

Hata kama atakuwa anakupenda kiasi gani, atakuvumilia siku za mwanzo lakini kadiri mnavyokwenda atajitoa kwako taratibu. Hii ni kwa sababu mwanaume atahisi siku akija kuwa hana kitu anaweza kuibiwa na wenye fedha.

Muongeaji sana

Mwanamke muongeaji sana asiyekuwa na staha, mwanamke ambaye hawezi kumvumilia mwanaume pale anapokuwa akimsema kwa jambo f’lani kwa nia ya kutaka maelewano ni tatizo.

Namzungumzia yule ambaye muda wote anataka kushindana na mume/ mpenzi wake katika kuongea, yaani kuonesha kuwa hajakosea, anaonewa au na yeye yumo kwenye kuongea, huyu hawezi kumshika mtu wake.

Mwanamke anayeijenga ndoa yake anatakiwa kuwa chini pale mwanaume anapokuwa anapaza sauti, akishapoa na wote mmepoa. kama una dukuduku lako ongea naye taratibu.

Haiwezekani mume na mke kuwa juu hasa mnapokuwa kwenye mgogoro, inatakiwa mwanamke kumsoma mume wake au mpenzi wake kwa wakati huo.

Mwanamke kiguu na njia

Sifa ya mwanamke ni utulivu, kama wewe mwanamke una tabia za kupenda kwenda kila unaposikia ngoma au sherehe, wanaume wengi huwa hawapendezwi na tabia hii. Basi kuwe na sababu ya wewe kutoka si kila shughuli ikuhusu wewe.

Wapo ambao hukatazwa na waume zao na kulazimisha kwenda ilimradi tu aonekane naye hajapitwa na sherehe huku akiwa amevaa sare. Kama una tabia hiyo jiangalie.

Wivu wa kupindukia

Mwanamke mwenye wivu wa kupindukia humfanya mwanaume kukosa amani kwani hata awapo kazini kwake mwanamke atataka kumfuatilia na kumnyima uhuru.

Hawa wenye tatizo hili huachwa na wanaume wao haraka kwani wengi hawapendi kuonewa wivu wa hivyo, wengine huuita wivu wa kijinga.

Itaendelea wiki ijayo.

Leave A Reply