The House of Favourite Newspapers

Man United Wakutana Na Cavani

0

UONGOZI wa Klabu ya Manchester United umekutana na staa wa timu hiyo, Edinson Cavani kuona wanamshawishi kuendelea kusalia ndani ya kikosi hicho.

 

Cavani anatarajiwa kumaliza mkataba wake ndani ya United, Juni 2021 baada ya kusajiliwa kwa mwaka mmoja.

Mkurugenzi wa soka mpya wa Man United, John Murtough na Mtendaji Mkuu, Ed Woodward walikutana na Cavani kujadili hatma yake pamoja na mchezaji mwenyewe.

 

Hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa huenda, Cavani akatimka ndani ya kikosi kujiunga na Boca Junior.

Hata hivyo kumekuwa na taarifa pia kuwa Cavani amekuwa hana furaha kutokana na kitendo cha kufungiwa na FA mwezi Januari mwaka huu baada ya kupost neno ‘Negrito’ ambalo lilidaiwa la kibaguzi.

Ole Gunnar Solskjaer amesisitiza kuwa yeye anataka kuendelea kufanya kazi na Cavani hivyo anaamini mazungumzo yatamfanya asalie hapo.

 

Cavani anafahamu kuwa Man United ina mpango wa kuleta straika mwingine ndani ya kikosi hicho.Imeelezwa kuwa viongozi kwa sasa wanapambana kuona anasalia hapo, kwani Marcus Rashford anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa bega mwishoni mwa msimu kwa maana hiyo anaweza kutoanza msimu mpya.Staa huyo alijiunga na timu hiyo, Oktoba mwaka jana na amecheza mechi 26 katika michuano yote akifunga mabao saba.

Leave A Reply