Manchester United OUT Ligi ya Mabingwa, Yapigwa 3-2
NAHODHA wa Klabu ya Manchester United Harry Maguire amesema kuwa hawakustahili kufungwa usiku wa kuamkia leo mabao 3-2 dhidi ya RB Leipzig kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
United ilianza kuokota nyavuni bao mapema dakika ya 2 kupitia kwa Angelino na lile la pili lilifungwa dakika ya 13 na Amadou Haidara na kuwafanya waende mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili United iliokota nyavuni bao la tatu kupitia kwa Justin Kluivert dakika ya 69 na United walipata penalti dakika ya 80 iliyofungwa na Bruno Fernandes na lile la pili walipewa zawadi baada ya Ibrahima Konate kujifunga dakika ya 82.
Kichapo hicho Uwanja wa Red Bull Arena kinawafanya United chini ya Kocha Mkuu, Ole Gunnar kufungashiwa virago kwa kuwa walikuwa wanahitaji sare ili wajihakikishie nafasi ya kufuzu 16 bora ndani ya kundi H ila mambo yalikuwa magumu kwao.
Maguire amesema:”Tumeumia kutolewa na hatukupaswa kufungwa lakini kwa kuwa ni matokeo hatuna chaguo,”.
MATCH FACTS
RB Leipzig: Gulacsi, Mukiele, Konate, Orban, Angelino (Halstenberg 87), Sabitzer, Haidara, Kampl (Adams 75), Nkunku, Forsberg (Poulsen 56), Olmo (Kluivert 56).
Subs not used: Tschauner, Sorloth, Martinez, Martel, Wosz.
Goals: Angelino, 2, Haidara 13, Kluivert 69.
Booked; Mukiele, Sabitzer, Adams, Kluivert
Man Utd: De Gea, Wan Bissaka (Fosu-Mensah 77), Lindelof (Tuanzebe 78), Maguire, Shaw (Williams 61), McTominay, Matic (Pogba 61), Greenwood, Bruno Fernandes, Alex Telles (Van de Beek 46), Rashford.
Subs not used: Bailly, Mata, Grant, Lingard, James, Ighalo, Henderson.
Goals: Fernandes 80 (pen), Pogba 82
Booked: Lindelof, Maguire, Shaw, Williams, Fernandes
Referee: Antonio Miguel Mateu Lahoz (Spain)