MANCHESTER UNITED YAENDELEA KUGAWA DOZI TU, YATUPIA 4-0
Manchester United imeendelea kuwa na mwanzo mzuri katika Ligi Kuu ya England ‘Premier League’ baada ya kupata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Swansea City.
Man United sasa imefikisha pointi sita katika michezo miwili na imefunga mabao 8.
Waliofunga mabao katika mchezo huo ni beki Eric Bailly aliyefunga bao lake la kwanza akiwa ndani ya kikosi hicho, straika Romelu Lukaku alifunga bao moja na kumfanya afikishe mabao matatu ndani ya michezo miwili, Paul Pogba na Anthony Martial wakamalizia kazi hiyo.
Mchezo ujao wa Manchester United utakuwa ni dhidi ya Leicester City kwenye Uwanja wa Old Trafford, Jumapili ijayo.
Swansea: Fabianski, Fernandez, Bartley (Routledge 67), Mawson, Roque (Narsingh 67) , Naughton, Fer, Carroll, Olsson, Abraham (McBurnie 82), Ayew.
Subs: van der Hoorn, Nordfeldt, Rangel, Fulton.
Booked: Fer
Man Utd: de Gea, Valencia, Bailly, Jones, Blind, Pogba, Matic, Mata (Fellaini 75), Mkhitaryan (Herrera 85), Rashford (Martial 75), Lukaku.
Subs: Romero, Lindelof, Smalling, Lingard.
Booked: Pogba
Goal: Bailly 45, Lukaku 80, Pogba 82, Martial 84.
Referee: Jon Moss (W Yorkshire)
Attendance: 20,862