The House of Favourite Newspapers

Manji ampiga bao Dangote Afrika

0

MANJI

Mwenyekiti wa Makampuni ya Quality Group, Yusuf Manji.

Mwandishi Wetu,Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Makampuni ya Quality Group, Yusuf Manji ameibuka mshindi wa tuzo maarufu ya Mfanyabiashara Gwiji Duniani.

Manji ambaye ni mwenyekiti wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga, ameibuka mshindi wa tuzo hiyo na kuwashinda mabosi wengine kama bilionea namba moja Afrika, Aliko Dangote wa Nigeria.

Kwa mujibu wa Mtandao wa Business Forum, Mwenyekiti huyo amekuwa kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kushinda tuzo hiyo ambayo awali walikuwa wakichukua matajiri wengine wakubwa na maarufu kutoka katika Mabara ya Amerika, Ulaya na Asia.

Msemaji wa Quality Group, Smitha Swamy jana alithibitisha Manji kushinda tuzo hiyo, lakini akasema atakuwa tayari kulizungumzia hilo, leo.

“Ni kweli, lakini leo (jana) nimebanwa. Nitalizungumzia hilo kesho (leo),” alisema.
Baadhi ya waliowahi kutwaa tuzo hiyo ni Mwenyekiti wa Emirates Group, Sheikh Ahmed bin Saeed Al Maktoum inayomiliki Kampuni ya Ndege ya Emirates inayozidhamini timu za Real Madrid, Arsenal, AC Milan na nyingine kubwa.

Wengine ni Mwenyekiti wa Emmar Properties, Mohammed Alabbar pia bilionea kutoka India, Ratan Tata anayemiliki kampuni kubwa ya Emeritus of Tata Sons Ltd.

Pia bilionea namba tano kwa ubora duniani, Mukesh Ambani ambaye ni mwenyekiti wa Reliance Industries Ltd. Wengine ni Yingluck Shinawatra, Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand.

Pamoja na ushindi huo wa kishindo wa Manji dhidi ya matajiri wengine wakubwa Afrika na duniani kote, kampuni yake ya Quality Group imeshinda kuwa kampuni bora na yenye mpangilio wa uhakika kwa Bara la Afrika ikipewa Tuzo ya “Most Iconic Brand 2015”.

Leave A Reply